
Katibu mkuu wizara ya mambo ya nje wa Uganda, Balozi James Mugume, amesema kuwa Uganda haitishwi na vikwazo ilivyowekewa na Marekani kama hatua ya kupinga sheria yake kali kuhusu Ushoga.Kwa mujibu wa BBC, Balozi Mugume ameelezea kuwa serikali ya Uganda hata hivyo itafanya
mazungumzo na Marekani ili kufafanua hatua waliyochukua.Amesisitiza kuwa wataieleza Marekani sheria hiyo inapinga tabiaambayo sio ya kiafrika na maadili ambayo hayakubaliki katika jamii nyingi za
kiafrika.Serikali imesisitiza kuwa vikwazo hivyo havitakuwa na athari kubwa kwa nchi hiyo na pia imekanusha madai ya mashirika ya kijamii ,kuwatayari sheria hiyo imechochea ongezeko la dhuluma dhidi ya wapenzi wa jinsia moja
No comments
Post a Comment