Picha: Diamond na dancers wake wahojiwa kwa masaa Polisi Oyster Bay

IMG_7048
Diamond Platnumz akitoka nje ya kituo cha polisi Osyter Bay, katikati ni Chief Kiumbe
Diamond Platnumz pamoja na dancers wake, wamehojiwa kwa masaa kadhaa kwenye kituo cha polisi cha Oyster Bay jijini Dar es Salaam baada ya kuitwa kwenda kujieleza kutokana na kuvaa sare za jeshi la wananchi Tanzania, JWTZ, kwenye show ya Fiesta, kinyume cha sheria.
Hata hivyo Diamond aliiambia Bongo5 kituoni hapo kuwa hakuwa tayari kuzungumzia kile walichokuwa wakihojiwa na polisi. Awali kulikuwa na taarifa kuwa meneja wake, Babu Tale alishikiliwa katika kituo hicho kuanzia jana kabla ya kutoka Jumatano hii.
IMG_7049
Diamond na Chief Kiumbe wakiteta jambo

IMG_7050

IMG_7051

IMG_7052

IMG_7053
IMG_7054
Tags