AY amesema kuwa ukaribu alionao na msanii Mjamaica-Mmarekani, Sean Kingston ni zaidi ya urafiki wa kikazi kiasi ambacho wanachkuliana kama kama familia.
AY ameiambia Bongo5 kuwa mama yake Sean humchukulia kama mtoto wake na wanawasiliana mara kwa mara.
“Yaani huyu jamaa ananipa support asilimia 100 huwezi kuamini ni mtu ambaye si yeye tu hadi mama yake mwenyewe tunawasiliana, kwahiyo ni family yaani”. Alisema Ambwene
“Mama yake ananichukulia kama mtoto wake, hata kwenye Instagram yangu ana comment, halafu hii yote ni family ambayo mi nikienda L.A ndo watu wangu ambao hua nahang nao”.
Collabo ya AY na Sean Kingston iitwayo ‘Touch me Touch Me’ inatarajiwa kutoka November.
No comments
Post a Comment